UCHI ni ukamilifu usio hitaji ziada, tunazaliwa tukiwa uchi na kamilifu, wenye tunu na thamani isiyopimika, na yanye utofauti na kiumbe mwingine awae yote. Na katika ukamilifu huo, ndimo kumejaa matunda ambayo baadhi yake yanadhihirika katika hali na mali.
Ni watu wachache ambao wamefanikiwa kuyatofautisha mafanikio yao na hali yao ya uchi, wengi wanayatafsiri mafanikio kwa kigezo cha hali na mali.